Featured

    Featured Posts

    Social Icons


Loading...

Watanzania waishio South Africa wavamiwa.

Naomba nikushirikishe na wewe pia kwamba kuna mambo mengi na mazuri ndapi ya picha iliyopo hapo chini ibofye uone.
Hizi ni picha ambazo zinaonesha jinsi mtaa wa Watanzania ulivyovamiwa, na watu kupigwa sana huko nchini South Africa siku ya jana.

 Afrika Kusini ni nchi yenye uchumi mkubwa Afrika ambao umevutia Waafrika wengi kukimbilia huko kwa ajili ya kufanya kazi kama za Udereva, uuzaji mafuta kwenye vituo vya mafuta pamoja na kazi nyingine mbalimbali za kijamii nchini hapo. 


 Taarifa kutoka kwenye mji wa Pretoria ni kwamba Watanzania ambao wanamiliki na kufanya biashara mbalimbali zikiwemo za Maduka na wale wanaomiliki hoteli, wamevamiwa wakiwa kwenye mali zao na kufanyiwa uharibifu na nyingine kuchomwa moto. 

 Ni kundi la watu ambalo linaendeleza uvamizi huu ambapo linawashutumu Watanzania hawa kuhusika na biashara ya dawa za kulevya, yani kwa ufupi Watanzania wanasema hata kama kweli wangekua wanafanya hii biashara, walio na mamlaka ya kuwavamia ni Polisi na sio hao raia wa kawaida. 


 Inaaminika kuwa kundi hili lina sehemu kubwa ya madereva Taxi wazawa wa nchi hiyo ambao wamekua wakiumizwa na jitihada za raia wa kigeni wa Nigeria na Watanzania ambao wamejazana kwenye mtaa wao wakimiliki maduka mbalimbali yakiwemo ya nguo, vipodozi pamoja na hoteli. 


 Tayari balozi wa Tanzania amekutana na Watanzania hao na kuahidi kulifatilia jambo hilo kwa ukaribu zaidi na kubaini chanzo cha tatizo hilo. Katika tukio hilo ni Watanzania watano ambao wamejeruhiwa na watatu bado wako hospitali na mmoja kati yao kavunjika mkono, na mmoja kapigwa akiwa amepigwa sana sehemu ya kichwani. 


 Kabla ya Watanzania wengine kuwahi kufunga maduka yao, maduka matatu ya Watanzania pamoja na hoteli mbili zinazomilikiwa na Watanzania zilivamiwa na watu wote walichuchukuliwa simu zao, huku watu wakiendelea kupigika sana.


 Baada ya mda mfupi polisi walipokuja hakuna chochote kilichofanyika zaidi ya kuchukua maelezo kwa wahanga wa tukio hao kisha kuondoka zao katika maeneo yao ya kazi. 


Picha hizi zote zilipigwa na Mtanzania akiwa anakimbia baada ya kufanikiwa kufunga duka lake na kuweza kujinusuru.

Pia waweza kupata taarifa mbalimbali za kila aina zinazoifikia http://mutalemwa-masgider.blogspot.com wakati wowote, kwa ku jiunga na mimi katika facebook na twitter ili nikutumie kila kitu kinacho jiri ndani na nje ya mipaka ya Tanzania kwa masaa 24 kila siku.
Usikose kuangalia Movies mbalimbali kutoka kila kona ya dunia, bofya kwenye picha iliyopo hapo chini kuona izo muvies
Nobody is a total failure if he dares to try to do something worthwhile. Tough times never last, but tough people do. The place broke up with applause. Those thirty - five hundred farmers who had lost hope and had battled depression found that hope.

Share habari hii kadri uwezavyo.

Contact us on mutalemwa.oesmo@gmail.com. Powered by Blogger.
© Copyright Mutalemwa Blog
Back To Top