Manchester United jana iliendeleza uteja wake kwa wapinzani wao Manchester City baada ya kukubali kipigo cha mabao 3-0 katika mchezo uliopigwa kwenye dimba la Old Trafford, jana usiku.
Matokeo ya mchezo huo yalitengeneza rekodi nyingine mbovu za Manchester United chini ya kocha David Moyes na zipo kama ifuatavyo
Kipigo cha jana usiku kinaamanisha United sasa imepoteza mechi ugenini na nyumbani dhidi ya Liverpool na Manchester City ndani ya msimu mmoja haijawahi kutokea hii huko nyuma.
Man United mpaka sasa imefungwa mechi 10 katika premier league, idadi kubwa zaidi katika historia yao.
Pia kati ya mechi hizo 10 sita wamefungwa Old Trafford, haijawahi kutokea katika miaka 12 iliyopita United kufungwa mechi sita za ligi kuu kwenye uwanja wake wa nyumbani.
Mpaka sasa United imecheza 13 dhidi ya timu 9 za juu katika msimamo wa ligi na kati ya hizo imeshinda mechi 1 tu dhidi ya Arsenal.