Leo ikiwa ni tarehe 4/5/2015 nyakati za hasubuhi kabisa. Kama inavyo onekana kwenye picha abilia wanaotegemea usafili wa daladala kuelekea maeneo mbalimbali ya jiji la Dar es salaam wakiwa wamejazana vituoni wakisubili magari bila mafanikio.
Katika eneo hili magari yaliyo onekana yakitoa huduma japo kwa uchache ni magari ya Temeke vs K/Koo, Buguruni vs Mbagala rangi 3, Temeke vs Msewe pamoja na magari ya UDA, uku bodaboda zikionekana kufanya kazi.
Sikubahatika kuyaona magari ya Mbagala rangi tatu vs Kariakoo, Ubungo Mawasiliano vs Mbagala rangi 3 pamoja na Mbagala vs Posta kwa mda masaa manne niliyokaa maeneo hayo.
Pia abilia wanarani kitendo cha madreva kugoma pasipo na sababu za msingi maana wanakwamisha kazi zao na kuwarudisha nyuma kimaendeleo.
Ikumbukwe kuwa leo ni mala ya pili madreva wa dar es salaam kugoma ndani ya mwaka 2015, pia mpaka sasa bado haijafahamika nini hatima ya mgomo huu wa madreva.
Abilia wanapata shida sana nyakati kama hizi ambapo watu utembea kwa mguu kutoka manyumbani kwao mpaka kwenye maeneo yao ya kazi na nyakati za kurudi makwao hutembea vilevile.
Kwa habari za Matukio Kitaifa, Kimataifa, Michezo na Burudani, Ungana nami kupitia Link zifuatazo hapo chini.
In order you follow me just click one of the Icon Button above.