Serikali imesema kuwasili kwa mabehewa mapya ya treni 72 kutaiwezesha kampuni ya TRL kuimarisha safari za kusafirisha abiria kwenda Mikoa ya Mwanza na Kigoma mara tatu kwa wiki.
Pia kutokana na ubora wa mabehewa hayo,TRL inataraji kuanzisha treni maalum kutoka Dar es salaam kwenda Mwanza na Kigoma itakayosimama kwenye vituo vikubwa pekee.
Mwakyembe alisema treni hiyo itakua na uwezo wa kusafiri kwa muda mfupi zaidi kulinganisha na safari za sasana alisema lengo la Serikali ni kuimarisha usafiri wa reli na kuifanyaTRL ijiendeshe pasipo kutegemee ruzuku kutoka Serikalini.
Aliongeza kuwa mabehewa hayo yalinunuliwa na Serikli ikiwa ni sehemu ya utekelezaji mpango wa matokeo makubwa sasa,ambapo mabehewa 274 yamekwishanunuliwa na kugharimu zaidiya bilioni200.
![](https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgqkfvdsCQnPtVtdB1BRo8WNnIXPkLftFAgnwnEsIn6wi5e6a3eWRGwII7wh1RRZiR7YnhR6IfHZu2S-L5TKd4i4JeqIXAZnEeqqNhmqdzjNYA4Q76BTKpB9MmvWIsr0dnAZXNg5DJSgT0/s200/FLASH+NECTA.gif)
Kwa habari za Matukio Kitaifa, Kimataifa, Michezo na Burudani, Ungana nami kupitia Link zifuatazo hapo chini.
In order you follow me just click one of the Icon Button above.