Ripoti mpya ya kimataia kuhusu hali ya Utumwa Afrika duniani imeitaja Tanzania kuongoza Afrika Mashariki kwa kuwa na watu zaidi ya 350,000 wanaotumikishwa katika maeneo mbalimbali nchini kinyume na utaratibu.
Waziri wa Maendeleo,jinsia na Watoto Sophia Simba alisema ni kweli kuwa wafanyakazi wa ndani wanatumikishwa sana hapa nchini ukilinganisha na nchi nyingine.
Ripoti hiyo ijulikanayo kama ‘The Global Slavery Index 2014′ iliyotolewa nchini Australia inaonyesha kuwa Tanzania inashikilia nafasi ya 14 barani Afrika na kuwa ya 33 duniani.
Uganda ndiyo inayoshikilia nafasi ya pili kwa kuwa na watu 135,000 ikifatiwa na Rwanda 83,600,Burundi 72,300 huku Kenya ikiwa na watumwa 64,900.
![](https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgqkfvdsCQnPtVtdB1BRo8WNnIXPkLftFAgnwnEsIn6wi5e6a3eWRGwII7wh1RRZiR7YnhR6IfHZu2S-L5TKd4i4JeqIXAZnEeqqNhmqdzjNYA4Q76BTKpB9MmvWIsr0dnAZXNg5DJSgT0/s200/FLASH+NECTA.gif)
Kwa habari za Matukio Kitaifa, Kimataifa, Michezo na Burudani, Ungana nami kupitia Link zifuatazo hapo chini.
In order you follow me just click one of the Icon Button above.