Katika kuhakikisha uchochezi unaoharibu amani ya nchi Unathibitiwa wakati wa uchaguzi wa Serikali za mitaa,Serikali imeagiza Mamlaka ya sekta ya Mawasialino nchini TCRA kuja na mwongozo wa Mamlaka za simu katika kuthibiti ujumbe mfupi kwa njia ya simu.
Waziri wa Mawasiliano Makame Mbarawa alisema ujumbe mfupi kwenye simu usipothibitiwa unaweza kuleta madhara makubwa wakati wa uchaguzi.
“TRCA mje na mwongozo wa makampuni ya simu hasa kuhusu ujumbe wa simu maana kama itaachwa hivi hivi wakati wa uchaguzi itakua ni hatari,Kenya ilifanya hili na ikafanikiwa,”alisema Mbarawa.
Tayari TCRA imeandaa miongozo ya namna ya kuripoti na kuandaa vipindi wakati wa uchaguzi kwa upande wa sekta ya utangazaji na wamiliki wa mitandao ya kijamii.
![](https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgqkfvdsCQnPtVtdB1BRo8WNnIXPkLftFAgnwnEsIn6wi5e6a3eWRGwII7wh1RRZiR7YnhR6IfHZu2S-L5TKd4i4JeqIXAZnEeqqNhmqdzjNYA4Q76BTKpB9MmvWIsr0dnAZXNg5DJSgT0/s200/FLASH+NECTA.gif)
Kwa habari za Matukio Kitaifa, Kimataifa, Michezo na Burudani, Ungana nami kupitia Link zifuatazo hapo chini.
In order you follow me just click one of the Icon Button above.