Harufu ya kuisha kwa mgogoro baina ya Zitto Kabwe na Chama chake cha Chadema inanukia,lakini Mbunge huyo wa Kigoma Kaskazini anataka kuwepo na mazungumzo kubaini tatizo ili atakayebainika kuwa alifanya makosa awe tayari kuomba radhi hadharani.
Zitto alikiri Mbungeni kuwa amekua akimis harakati zilizokua zikifanywa na vyama vya upinzani wakati wa Bunge maalum la Katiba,harakati zilizozaa Umoja wa Katiba ya wananchi na kufurahia kuhudhuria mara kwa mara vikao vya umoja huo.
Zitto ambaye Novemba mwaka jana alivuliwa nyadhifa ndani ya Chama hicho kwa madai ya kukihujumu Chama alifanikiwa kulinda uanachama wake baada ya kufungua kesi mahakamani na kufanikiwa kupata amri ya kuzuia asijadiliwe..
“Ukweli wangu ndani ya Chadema ni nini?mimi ninaona sina kosa lolote ndani ya Chadema,ninachotaka mimi nielezwe ukweli bila chembe ya shaka,Nitakua tayari kuomba radhi hadharani kama ikibainika nilifanya makosa na kama ikibainika Chama kilifanya makosa,nacho kiwe tayari kuomba radhi hadharani na ukweli uwe mbele katika maridhiano”alisema Zitto.
![](https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgqkfvdsCQnPtVtdB1BRo8WNnIXPkLftFAgnwnEsIn6wi5e6a3eWRGwII7wh1RRZiR7YnhR6IfHZu2S-L5TKd4i4JeqIXAZnEeqqNhmqdzjNYA4Q76BTKpB9MmvWIsr0dnAZXNg5DJSgT0/s200/FLASH+NECTA.gif)
Kwa habari za Matukio Kitaifa, Kimataifa, Michezo na Burudani, Ungana nami kupitia Link zifuatazo hapo chini.
In order you follow me just click one of the Icon Button above.