Featured

    Featured Posts

    Social Icons


Loading...

UJUMBE MAALUM KUTOKA KWA MHE.EDWARD LOWASSA, BOFYA HAPA

Naomba nikushirikishe na wewe pia kwamba kuna mambo mengi na mazuri ndapi ya picha iliyopo hapo chini ibofye uone.

Nina furaha kutimiza mwaka mmoja toka nilipojitoa CCM na kujiunga na CHADEMA.Uamuzi ule haukuwa rahisi,lakini kwa ushupavu, ujasiri na mwongozo wa Mungu nilifanya hivyo.Nilifanya uamuzi wa kihistoria katika nchi yetu.

Najivunia kwa uamuzi ule,kwani umewafungua macho watanzania wengi na kuimarisha demokrasia.Nimeingia CHADEMA nimewakuta viongozi na wanachama waliyo na moyo wa dhati wa kuliletea maendeleo taifa lao KIVITENDO.Najihisi mwenye furaha kubwa na raha kuwa katika upande huu.

Watanzania bado wanataka mabadiliko na imezidi kuthibitika kuwa hawawezi kuyapata ndani ya CCM .Watanzania wanataka sera na mtu mbadala wa kuongoza mabadiliko hayo.Vyote hivyo watavipata ndani  ya CHADEMA na UKAWA kwa jumla.

Nawahakikishia watanzania na wana UKAWA kwa jumla,kuwa sasa hivi NINA ARI,NGUVU NA HAMASA kubwa kuliko wakati mwengine wowote.

Kwa wale wenzangu waliyobaki CCM na wanaoniunga mkono,tuendelee kushikamana na kunipatia taarifa kwa hatma ya nchi yetu.Nawashukuru watanzania kwa kuendelea kuniunga mkono mimi na wenzangu ndani CHADEMA.

Edward Ngoyai Lowassa
Mjumbe wa kamati Kuu CHADEMA
Waziri Mkuu mstaafu.

Usikose kuangalia Movies mbalimbali kutoka kila kona ya dunia, bofya kwenye picha iliyopo hapo chini kuona izo muvies
Nobody is a total failure if he dares to try to do something worthwhile. Tough times never last, but tough people do. The place broke up with applause. Those thirty - five hundred farmers who had lost hope and had battled depression found that hope.

Share habari hii kadri uwezavyo.

Contact us on mutalemwa.oesmo@gmail.com. Powered by Blogger.
© Copyright Mutalemwa Blog
Back To Top