Featured

    Featured Posts

    Social Icons


Loading...

WAKULIMA WA KIJIJI CHA ISAKAMALIWA WAITUPIA LAWAMA SERIKALI, BOFYA HAPA KUJUA ZAIDI

Naomba nikushirikishe na wewe pia kwamba kuna mambo mengi na mazuri ndapi ya picha iliyopo hapo chini ibofye uone.

Wakulima wa kijiji cha Isakamaliwa kitongoji cha Magogo wilaya Igunga Tabora wameilalamikia serikali ya wilaya hiyo kushindwa kutatua mgogoro wa ardhi kati yao na wafugaji wanaotoka katika maeneo ya wilaya ya Kishapu mkoani Shinyanga, mgogoro ambao unafukuta kwa zaidi ya miaka miwili na kusababisha watu zaidi ya 200 kukimbilia kijiji jirani na kuishi maisha tegemezi.

Wakulima hao wapatao zaidi ya 200 wanaoishi nje ya makazi yao baada ya kufanyiwa vurugu na nyumba zao kuchomwa moto na watu wanaodhaniwa kuwa ni wafugaji wamepaza sauti zao na kuangua kilio mbele ya mkuu wa wilaya ya Igunga Bi. Zipora Pangani wakiiomba serikali kuingilia kati na kutatua mgogoro huo ili warudi katika maeneo yao na kuendelea na maisha ya kawaida.

Hali hiyo haikuathiri wakulima pekee bali hata vijana waliohitimu masomo ya elimu ya vyuo vikuu ambao walijikita katika kilimo cha mboga mboga nao wamejikuta wakiwa ni wahanga wa tukio hilo.

Licha ya serikali kutupiwa lawama kushindwa kutatua mgogoro huo uliodumu kwa muda mrefu mkuu wa wilaya ya Igunga Bi.Zipora Pangani ameeleza mikakati ambayo serikali imeamua kufanya ili kutatua mgogoro huo.
Tiba ya migogoro ya ardhi dhidi ya wakulima na wafugaji nchini bado haijapatikana  huku hali hiyo ikionekana kuendelea kuzorotesha nguvu kazi ya Taifa.

Usikose kuangalia Movies mbalimbali kutoka kila kona ya dunia, bofya kwenye picha iliyopo hapo chini kuona izo muvies
Nobody is a total failure if he dares to try to do something worthwhile. Tough times never last, but tough people do. The place broke up with applause. Those thirty - five hundred farmers who had lost hope and had battled depression found that hope.

Share habari hii kadri uwezavyo.

Contact us on mutalemwa.oesmo@gmail.com. Powered by Blogger.
© Copyright Mutalemwa Blog
Back To Top