Featured

    Featured Posts

    Social Icons


Loading...

JE WEWE UNA BLOG AU WEB SITE? BASI SOMA HII INAUSU FAIDA ZA ADSENSE

Naomba nikushirikishe na wewe pia kwamba kuna mambo mengi na mazuri ndapi ya picha iliyopo hapo chini ibofye uone.

Mimi ni mtumiaji wa google adsense, kupitia adsense nimeweza kupata kipato cha kuendesha maisha
yangu kwa njia mbalimbali , kama ujenzi wa nyumba na uendeshaji wa
biashara nyingine kupitia kipato hicho tu .

Watu wengi wanapenda kujiunga na adsense na wengine walijiunga
wakakata tamaa au hata wengine akaunti zao kufungiwa kutokana na
kukiuka masharti kadhaa ya google adsense , mimi mwenyewe nilifungiwa
mara 3 hivi na nilipoteza zaidi ya milioni 5 za kitanzania .

Hili ni somo fupi kwa wale wanaopenda kujiunga na adsense au ambao
wameshajiunga lakini wanataka kupata faida zaidi .

            Google Adsense ni nini ?

Google adsense ni mfumo wa matangazo wa Google ambao unamwezesha mtu
kitangaza bidhaa zake kwa kipato alichotacho na kumwezesha mwenye
tovuti au blogu kufaidika kutokana na matangazo ya adsense kuonekana
kwenye blogu yake au tovuti yake .

Kwa lugha rahisi tunaweza kuita ppc Pay Per Click , Lipa kwa Click au
mguso mmoja kwenye tangazo husika, mimi mwenye blogu hela utakuja
kwangu kama mtu aligusa au gonga tangazo alilioona kwenye blogu yangu
na yule aliyetangaza bidhaa zake kwenye google hela ndio inakatwa
kutokana na click hiyo .

Mimi nina blogu nyingi ambazo nimejisajili na google adsense ,
ukiingia kwenye blogu hizo utaona matangazo yanaonekana yale matangazo
sijaweka mimi na sijuani na walioweka matangazo hayo mimi yangu ni
blogu na nafasi ya kutangaza niliyoiweka kwenye blogu .

Unajiungaje na Adsense ?

Adsense ni mali ya Google ni lazima au vizuri uwe na barua pepe ya
gmail ambayo ni ya google au nyingine ambayo itakuwezesha kuweza
kusajili adsense kwa urahisi lakini ni vizuri iwe imesajiliwa google .

Usajili unakuwaje ?

Ukishasajili inachukuwa siku 15 kwa
tovuti yako au blogu yako kuangaliwa kama inakidhi viwango vya google
adsense kama lugha ,picha ,maudhui ,rangi na copyrights .

Unaposajili unapewa CODE maalumu ambazo unaweza kuweka kwenye kurasa
za tovuti au blogu yako kwa ajili ya kuanza kuonyesha matangazo
mbalimbali .

Nikisema lugha nina maanisha utumie lugha zinazokubalika na adsense
kama kiingereza , kifaransa na nyingine za kimataifa Kiswahili
hakitakiwi labda uchanganye, kama blogu au tovuti yako ina picha chafu
haitakiwi , rangi zake ziwe nzuri zisiingilie maslahi ya matangazo ya
adsense na angalia milki ya vile unavyoweka .

Baada ya siku 15 inakuwaje ?

Baada ya siku 15 utapata email kama umekubaliwa au umekataliwa kama
imekataliwa unaweza kuangalia ulichokosea na kubalisha kwa kukata
rufaa unatakiwa ujaze appeal form ambayo nayo itaangaliwa kwa siku
15 .

Kama umekubaliwa basi unatakiwa kuingiza dola 100 au euro 70 , hela
hizi zinapatikana kutokana na matangazo yanayoonekana kwenye blogu au
tovuti yako , ukiwa na kipato hicho utatumiwa kadi yenye namba ya siri
ambayo utaingiza kwenye akaunti yako ili uweze kukamilisha usajili
wako wa adsense , mlolongo huu unaweza kuchukuwa miezi 2 hivi .

Unalipwaje ?

Inategemea umechagua mfumo gani wa kulipwa , kuna mifumo 3 hivi
inayojulikana zaidi.

a)Cheki – njia hii ilikuwa inatumika zaidi zamani hata sasa hivi kwa 

baadhi ya nchi na wale wanaopenda , kwa wale wa afrika inachukuwa siku
7 kupata cheki yako hapo utakatwa euro 17 kwa ajili ya kusafirisha
cheki hiyo ,halafu unatakiwa kuingiza cheki kwenye akaunti yako ya
benki ambapo inachukuwa siku 21 kulipwa au zaidi ya hapo – benki
nyingine hazikubali cheki hizi kwahiyo wanaweza kukataa , kama
ikikubali benki itakata hela ya kuprocess cheki .

b) Uhamisho wa Benki – Njia hii pia ni nzuri lakini kuna hela Fulani
unakatwa kwa ajili ya kuhamisha hela kutoka nchi moja kwenda nyingine
kwa njia ya benki na sio benki zote zenye huduma hii na inategemeana
na kiwango cha hela inayotumwa kama ni ndogo sana inaweza kuwa tabu
kidogo .

c) Western union – Hii ndio bora na ya haraka zaidi mara nyingi
inalipwa kila mwisho wa mwezi unaofuatia kama ulipata dola 600 mwezi
wa 3 utalipwa mwezi wa 4 mwishoni baada ya mahesabu kukamilika na
baada ya kukatwa kodi na masuala mengine muhimu .

NINI KISICHOTAKIWA ?

1 – Huduma nyingine za Matangazo , Kwa sababu adsense ni Pay Per Click
ni bora usiweke matangazo mengine ya PPC kwa sababu yataingiliana na
maslahi ya adsense unaweza kufungiwa au kuweka huduma nyingine za
matangazo ambazo zinaweza kuzorotesha huduma za matangazo ya adsense .

2 – Kulazimisha watu kugonga au click au wewe mwenyewe kufanya hivyo ,
hutakiwi kulazimisha watu kugonga matangazo ili ujiongezee
kipato ,waache waangalie na kuamua wenyewe , kazi yako iwe ni kuweka
taarifa za kutosha kwenye blogu au tovuti yako zinazovutia watu
kutembelea na kuvutia watu wa masoko kupitisha matangazo yao kwenye
kurasa zako.

Hiyo namba moja ndio ya kwanza na muhimu zaidi nyingine ni Lugha ,
haki miliki , picha chafu na rangi nzuri kwenye kurasa zako ambazo
zitafanya matangazo kuonekana vizuri .

FAIDA KWA MWENYE BLOGU TOVUTI

Kutegemeana na aina ya blogu yako na maudhui lakini blogu au tovuti
ili iweze kupata zaidi ya dola 15 kwa siku inatakiwa angalau kuwa na
watembeleaji wa siku moja zaidi ya alfu 3000 , wanaotembelea toka nchi
zinazoendelea na kuclick toka nchi za ulaya ndio wenye fedha na
kuwezesha kulipwa vizuri zaidi kuliko nchi za afrika .

Kwa Tanzania blogu ya kawaida yenye watembeleaji kati ya 2000 au 4000
kwa Tanzania inatakiwa iwe na shilingi laki 9 kwa mwezi mmoja au zaidi
kama kipato chake

FAIDA KWA WATANGAZAJI/WAFANYABIASHARA.
Utangazaji kwa kupitia adsense ni rahisi na fedha yako inaenda
kihalali na ni rahisi kutokana na bajeti yako kama umepanga kutangaza
kwa laki 1 kwa mwezi na unataka tangazo lako lionekane Tanzania pekee
basi kwa kupitia adsense hiyo inawezekana kama unataka lionekana kwa lugha ya kiingereza pekee na lionekane japan au korea hilo
linawezekana ni wewe kuamua na kufanikisha hilo kupitia adsense .

Kama wewe ni mfanyabiashara huhitaji kuhangaika kutafuta blogu au
tovuti kubwa kutangaza bidhaa zako ambako inaweza kuwa gharama zaidi
na kupata nafasi ni finyu , fikiria adsense ifanyie kazi .

ADSENSE INAWEZA KUWA AJIRA TOSHA ?
Inategemea na mipango yako lakini adsense sio ya kuitegemea sana kama
usipofuata taratibu unaweza kufungiwa lakini kama ukifuata masharti na
kukaa nayo vizuri inaweza kuwa ajira yako inayokulipa vizuri na
kufanya maisha yako kwenda vizuri .

ADSENSE SIKU ZIJAZO .
Sasa hivi watu wanatumia simu za mikononi na vifaa vingine kwa ajili
ya kutembelea tovuti na blogu sio komputa kama zamani , kama ni
mtumiaji wa adsense jiandae kwa hilo hakikisha matangazo yako ni
mepesi na yanaweza kuonekana au kusomeka na watu wanaotuvmia vifaa
hivi na kukulipa vizuri bila usumbufu mwingine.

Usikose kuangalia Movies mbalimbali kutoka kila kona ya dunia, bofya kwenye picha iliyopo hapo chini kuona izo muvies
Nobody is a total failure if he dares to try to do something worthwhile. Tough times never last, but tough people do. The place broke up with applause. Those thirty - five hundred farmers who had lost hope and had battled depression found that hope.

Share habari hii kadri uwezavyo.

Contact us on mutalemwa.oesmo@gmail.com. Powered by Blogger.
© Copyright Mutalemwa Blog
Back To Top