Featured

    Featured Posts

    Social Icons


Loading...

WAANGALIZI WA UCHAGUZI ZANZIBAR WASEMA HAWATASHIRIKI KATIKA ZOEZI HILO, ZAIDI BOFYA HAPA

Naomba nikushirikishe na wewe pia kwamba kuna mambo mengi na mazuri ndapi ya picha iliyopo hapo chini ibofye uone.

Muungano wa Waangalizi wa Ndani wa Uchaguzi (Cemot) umesema hautashiriki katika uangalizi wa uchaguzi wa marudio Zanzibar utakaofanyika Machi 20 mwaka huu kutokana na kukabiliwa na ukata.

Cemot ni umoja wa taasisi za waangalizi wa ndani wa uchaguzi inayohusisha Kamati ya Uangalizi wa Uchaguzi (Temco) na Muungano wa taasisi zisizo za kiraia za kusimamia uchaguzi (Tacceo) ambazo zilitumia waangalizi katika Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 25, mwaka jana.

Akizungumza na waandishi wa habari Arusha katika warsha ya mrejesho wa taarifa ya waangalizi wa ndani wa Uchaguzi Mkuu, Mwenyekiti mwenza wa Cemot, Martina Kabisama alisema fedha zote zilitumika katika uchaguzi uliopita.

“Kwenda kuangalia uchaguzi ni jambo linalohitaji rasilimali, hivyo hatutakwenda Zanzibar katika uchaguzi wa marejeo kwa kuwa tulikuwa hatujaandaa andiko la kupata fedha za uchaguzi huo,” alisema.

Kabisama alisema Cemot ilikuwa na waangalizi wa muda mfupi 9,400 na wengine 350 waliotoka Tacceo na Temco.

Mwangalizi wa ndani wa Uchaguzi Mkuu kwa Tanzania Bara na Visiwani, Dk Alexander Makulilo alisema Cemot ilifanya kazi kubwa katika uangalizi na imeandaliwa taarifa inayoonyesha mahitaji ya maboresho katika chaguzi zijazo.

Dk Makulilo ambaye anaongoza timu ya uandishi wa taarifa ya Cemot, alisema uchaguzi wa Zanzibar uliopita ulikwenda vizuri licha ya kuwapo dosari kidogo sawa na Tanzania Bara.

Alisema Tume ya Uchaguzi Zanzibar (ZEC) na mashirika yasiyo ya kiserikali, walifanya kazi ya kutoa elimu ya wapigakura, tofauti na Tanzania Bara.

Pia alisema visiwani humo polisi walitekeleza vizuri wajibu wao tofauti na Tanzania Bara.

Dk Makulilo alisema asilimia 87 ya waangalizi wa Zanzibar walieleza polisi walifanya kazi nzuri kwa asilimia 65 kutokana na kusimamia vema uchaguzi.


Usikose kuangalia Movies mbalimbali kutoka kila kona ya dunia, bofya kwenye picha iliyopo hapo chini kuona izo muvies
Nobody is a total failure if he dares to try to do something worthwhile. Tough times never last, but tough people do. The place broke up with applause. Those thirty - five hundred farmers who had lost hope and had battled depression found that hope.

Share habari hii kadri uwezavyo.

Contact us on mutalemwa.oesmo@gmail.com. Powered by Blogger.
© Copyright Mutalemwa Blog
Back To Top