Featured

    Featured Posts

    Social Icons


Loading...

UCHIMBAJI MADINI KWENYE MACHIMBO YA MORAMU WASIMAMISHWA, ZAIDI BOFYA HAPA

Naomba nikushirikishe na wewe pia kwamba kuna mambo mengi na mazuri ndapi ya picha iliyopo hapo chini ibofye uone.

Na Woinde Shizza,Arusha
Mkuu wa wilaya ya Arusha Fadhili Nkurlu amesimamisha shughuli za uchimbaji katika machimbo ya moramu katika kata ya Moshono Mkoani Arusha kwa kipindi cha mwezi mmoja kupisha wakandarasi kuweka sawa machimbo hayo ambayo yanachimbwa bila kufuata utaalamu hali ambayo inadaiwa inaweza kuhatarisha uhai wa maisha yao.

Katika kipindi cha mwaka 2013 machimbo hayo yaliuwa wachimbaji 13 hali ambayo ilimfanya waziri mkuu mstaafu Peter Pinda kuyafunga mpaka yatakaporekebishwa ndiyo wachimbaji hao waendelee na uchimbaji ingawa inadaiwa wachimbaji hao hawakufuata maagizo mpaka hivi sasa kwani waliendelea na shughuli za uchimbaji.

Akizungumza wakati akifunga machimbo hayo mkuu wa wilaya ya Arusha Fadhil Nkurlu alisema kuwa mazingira ya wachimbaji hao ni mabaya na yanahatarisha maisha yao kwa kiasi kikubwa na kwamba hawana utaalamu wa kutosha juu ya namna bora ya uchimbaji wa moramu hiyo mbali na kuchimba kinyemela toka kauli ya waziri mkuu kutamkwa.

Alisema kuwa ameamua kufunga machimbo hayo kutokana na oanagezeko kubwa la vifo linalosabibishwa na uchimbaji wa moramu usiozingatia sheria na kanuni.

Picha kutoka maktaba.
Naye kamishina msaidizi wa madini kanda ya kaskazini Elias Kadabila alichukuwa fursa hiyo kuwaomba wananchi kufuata maelezo ya mkuu wa wilaya ili waweze kuchimba kuchimba kwa usala ambapo alisema kuwa pia iatawasaidia kuepukana na maafa au vifo vinavyotokana na uchimbaji holela.

Aidha pia aliuomba uongozi wa mtaa pamoja na wachimbaji hao kutoa ushirikiano ili kuweza kuwapisha wakandarasi kutengeneza machimbo hayo kwa muda wa mwezi mmoja .

Gazeti hili pia liliweza kuzungumza na baadhi ya wachimbaji hao ambapo walisema kuwa hawakubaliani na agizo hilo la mkuu huyo kwakuwa uchimbaji huo ndiyo ambao unawafanya kumudu gharama za maisha na kusomesha watoto na kwamba serikali iangalie namna nyingine.

"kwakweli tunaomba serekali iangalie tena na tena swala hili kwani sisi wananachi ndio tunategemea maachimbo haya kwani ndio yanatusaidia tunaweza kula ,kusomesha watoto ,kujenga naweza sema kiujumla kuendesha maisha yetu"Alisema Lowayani Metili

Ipo haja ya wachimbaji hao kupisha marekebisho hayo yatakayofanywa na serikali kwa manufaa yao na uhai wao kwani kuendelea kuchimba wakati wanahatarisha maisha yao ni jambo la hatari Zaidi kwani wahenga wanamsemo usemao UHAI NI BORA KULIKO KIFO.
chanzo: Eddy blog

Usikose kuangalia Movies mbalimbali kutoka kila kona ya dunia, bofya kwenye picha iliyopo hapo chini kuona izo muvies
Nobody is a total failure if he dares to try to do something worthwhile. Tough times never last, but tough people do. The place broke up with applause. Those thirty - five hundred farmers who had lost hope and had battled depression found that hope.

Share habari hii kadri uwezavyo.

Contact us on mutalemwa.oesmo@gmail.com. Powered by Blogger.
© Copyright Mutalemwa Blog
Back To Top