Featured

    Featured Posts

    Social Icons


Loading...

KITUO CHA AFYA CHA MWENDAKULIMA KINAKABILIWA NA UPUNGUFU WA DAWA NA VIFAA TIBA, ZAIDI BOFYA HAPA

Naomba nikushirikishe na wewe pia kwamba kuna mambo mengi na mazuri ndapi ya picha iliyopo hapo chini ibofye uone.

Kituo cha afya cha Mwendakulima kinakabiliwa na upungufu wa dawa na vifaa tiba Shinyanga.

Kituo kipya cha afya cha Mwendakulima kilichoko wilayani Kahama katika mkoa wa Shinyanga kinakabiliwa na changamoto kubwa ya ukosefu wa dawa, vifaatiba pamoja na uhaba wa wahudumu hali ambayo inasababisha wananchi wanaoishi katika kijiji hicho kufuata huduma za kiafya katika vituo vilivyoko katika vijiji vya jirani wakihofia kutopata huduma bora katika kituo hicho cha afya cha Mwendakulima.

Akizungumzia changamoto zinazokikabili kituo cha afya cha Mwendakulima ambacho kimejengwa kwa ufadhili wa kampuni ya ACACIA inayomiliki mgodi wa dhahabu wa Buzwagi muuguzi mfawidhi katika kituo hicho Bi.Selestina mbezi ameiomba serikali kupeleka wahudumu wa afya katika kituo hicho pamoja na kukipatia dawa na vifaa tiba vya kutosha ili kuokoa maisha ya wananchi wanaotumia muda mrefu kufuata huduma za kiafya katika vituo vingine vilivyoko mbali na kijiji hicho hali inayotishia kupoteza maisha ya wagonjwa hususan wanawake wajawazito.

Kwa upande wake afisa mtendaji wa kata ya Mwendakulima Bw.Mussa Ibingo amedai kuwa serikali inatambua mchango wa kampuni ya ACACIA katika kufadhili miradi mbalimbali ya maendeleo ya jamii hivyo kuna kila sababu za kuhakikisha serikali inapeleka dawa na vifaatiba vya kutosha katika kituo hicho mapema iwezekanavyo huku baadhi ya wagonjwa waliokuwa wakitibiwa katika kituo hicho cha afya wakionyesha kuridhishwa na kuduma waliyoipata.

Usikose kuangalia Movies mbalimbali kutoka kila kona ya dunia, bofya kwenye picha iliyopo hapo chini kuona izo muvies
Nobody is a total failure if he dares to try to do something worthwhile. Tough times never last, but tough people do. The place broke up with applause. Those thirty - five hundred farmers who had lost hope and had battled depression found that hope.

Share habari hii kadri uwezavyo.

Contact us on mutalemwa.oesmo@gmail.com. Powered by Blogger.
© Copyright Mutalemwa Blog
Back To Top