MAHAKAMA
 ya Wilaya ya Ilala imesema mfanyabiashara na muimbaji wa muziki wa 
injili Emmanuel Mbasha ana kesi ya kujibu katika shtaka linalomkabili la
 ubakaji linalomkabili.
Katika shtaka hilo Mbasha anadaiwa kumbaka binti mwenye umri wa miaka 17 (jina linahifadhiwa) ambaye ni shemeji yake.
Mbele
 ya Hakimu Flora Mjaya, mwendesha Mashtaka Munde Kalombola alidai 
mahakama imemkuta Mbasha na hatia baada ya kupitia ushahidi wa pande 
zote mbili.

Mbasha
 ambaye ni mume wa muimbaji maarufu wa muziki wa injili Flora Mbasha 
anadaiwa kumbaka shemeji yake huyo kati ya Mei 23 na 25 mwaka huu eneo 
la Tabata ambako alikuwa akiishi naye.
Kesi
 hiyo ilianza kusikilizwa mahakamani hapo Septemba 5, 2013 ambapo binti 
huyo aliieleza Mahakama kuwa alibakwa na shemeji yake (Mbasha) kwa awamu
 mbili tofauti kabla ya kufanikiwa kukimbia.
Kwa
 mujibu wa Sheria ya Mwenendo wa Makosa ya Jinai ya mwaka 2003 sura ya 
20 kifungu cha 186, kifungu kidogo cha tatu, kesi hiyo inasikilizwa na 
Mahakama ya siri ili kulinda haki ya binti huyo.
Kesi
 hiyo itatajwa tena mahakamani hapo Julai 23, mwaka huu ambapo Mbasha 
anatakiwa kufika na mawakili wake ili kujitetea dhidi ya shtaka hilo.
Usikose kuangalia Movies mbalimbali kutoka kila kona ya dunia, bofya kwenye picha iliyopo hapo chini kuona izo muvies