Featured

    Featured Posts

    Social Icons


Loading...

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI NCHINI TANZANIA

Naomba nikushirikishe na wewe pia kwamba kuna mambo mengi na mazuri ndapi ya picha iliyopo hapo chini ibofye uone.
THE UNITED REPUBLIC OF TANZANIA
DIRECTORATE OF PRESIDENTIAL COMMUNICATIONS

Telephone: 255-22-2114512, 2116898
E-mail: ikulucommpress@googlemail.com
Website : www.ikulu.go.tz              
Fax: 255-22-2113425



PRESIDENT’S OFFICE,
STATE HOUSE, 
1 BARACK OBAMA ROAD, 
11400 DAR ES SALAAM. Tanzania.

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

Serikali ya Sweden inaridhishwa na kiwango cha maendeleo ya kiuchumi ya Tanzania kwa kipindi cha miaka 10 iliyopita na inadhamiria  kuinua ushirikiano  baina yake na Tanzania  ili kuleta maana zaidi katika maendeleo na kukua kwa uchumi kwa ujumla.


Waziri Mkuu wa Sweden Stefan Lofven amesema hayo jana tarehe 4, Juni, 2015 ofisini kwake alipokutana  na Rais Kikwete.  "Tumefikia kiwango kingine, tunahitaji kuanzisha awamu mpya ya Uhusiano wetu". Waziri Mkuu Lofven amesema.

Katika mazungumzo yao, viongozi hao wawili wamesema kuna umuhimu wa kuanzisha awamu nyingine ya maendeleo ambayo italeta maana zaidi ambapo Rais Kikwete amesema pamoja na ukweli kuwa uchumi wa Tanzania unakua kwa haraka, bado juhudi za kuondosha umaskini zinahitajika na zitafanikiwa kwa kuelekeza nguvu kwenye kilimo ambacho ndicho kinaajiri na kutegemewa na watanzania wengi zaidi hasa wanaoishi vijijini.

"Tumefikia awamu nyingine na ni awamu nzuri ya kudumisha uhusiano wetu, tunaweza kushirikiana kwenye nishati, kilimo ili kukuza uchumi zaidi".

Waziri Mkuu Lofven amemuambia Rais Kikwete na Rais Kikwete akaongeza
"Pamoja na misaada hiyo, awamu nyingine ya uhusiano baina ya Nchi mbili hizi inahitaji pia kuona makampuni ya kutoka Sweden yanawekeza nchini Tanzania na pia kukuza biashara baina ya nchi mbili hizi ili hatimaye Tanzania iweze kujitegemea zaidi na kupunguza kutegemea misaada".
Mapema kabla ya kufanya mazungumzo na Waziri Mkuu Rais Kikwete amekutana na Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Shirika La Maendeleo Sweden (SIDA) Bwana Torbjorn Pettersson ambaye amemueleza Rais kuwa; Sweden imeridhishwa na kiwango cha maendeleo na juhudi za kupunguza umaskini nchini Tanzania, Uchumi wa Tanzania umekua kwa wastani wa asilimia 7, katika kipindi cha miaka 10 iliyopita, Pato la Taifa limekua kutoka sola za kimarekani bilioni 14.4 hadi kufikia dola bilioni 49.2 za kimarekani, wakati Pato la Mtu kwa mwaka 2005 lilikuwa  dola 375 na mwaka 2014 limekua hadi dola 1038.

Rais Kikwete yuko nchini Sweden kuishukuru serikali ya Sweden na Watu wake kwa msaada wa maendeleo ambao umedumu tangu miaka ya 60. Nchi ya Sweden inaongoza kwa kuipatia  Tanzania misaada ya maendeleo na ni kutokana na misaada hiyo Rais Kikwete ameishukuru Sweden kwa kuiwezesha  Tanzania kuelekea kuwa Nchi yenye uchumi wa Kati (Middle Income Country) na kufuzu kutoka kundi la Nchi Masikini sana Duniani (Least  Developed Country).

Rais Kikwete pia amefanya mazungumzo na Spika wa Bunge la Sweden Bwana Urban Ahlin pamoja na viongozi wa vyama mbalimbali vya siasa nchini Sweden na kuwashukuru kwa misaada ya maendeleo kwa takribani miaka 50 sasa.

Viongozi hao wamempongeza Rais kwa kufanya ziara ya shukrani na kuwaaga kwani ni mara chache kwa viongozi wengi wa Kiafrika kuaga na kuondoka madarakani.

Imetolewa na;
Premi Kibanga,
Mwandishi wa Habari wa Rais Msaidizi

Stockholm - Sweden.

5 Juni, 2015.
Usikose kuangalia Movies mbalimbali kutoka kila kona ya dunia, bofya kwenye picha iliyopo hapo chini kuona izo muvies
Nobody is a total failure if he dares to try to do something worthwhile. Tough times never last, but tough people do. The place broke up with applause. Those thirty - five hundred farmers who had lost hope and had battled depression found that hope.

Share habari hii kadri uwezavyo.

Contact us on mutalemwa.oesmo@gmail.com. Powered by Blogger.
© Copyright Mutalemwa Blog
Back To Top