Featured

    Featured Posts

    Social Icons


Loading...

HIVI NDIVYO AJARI YA MKOANI MARA ILIVYOTOKEA SOMA..

Naomba nikushirikishe na wewe pia kwamba kuna mambo mengi na mazuri ndapi ya picha iliyopo hapo chini ibofye uone.


Baadhi ya majeruhi wa ajali hiyo ambao ni Waandishi wa Habari mkoani Mara Frolence Focus wa Mwananchi na Pendo Mwakembe wa Raia Tanzania wamenusulika kwenye ajali hiyo wakiwa kwenye basi la Mwanza Coach kutokea Musoma. 



Mashuhuda wamesema ajali hiyo imetokea leo majira ya saa 5 asabuhi, baada ya basi la Mwanza Coach lililokuwa likitokea Musoma kwenda Mwanza kugongana uso kwa uso na basi la J4 lililokuwa likitoka Mwanza kwenda Sirari. 



Zaidi ya watu 45 wanasadikiwa kufariki dunia na wengine wengi wakijeruhiwa vibaya baada ya mabasi mawili kugongana na kupinduka katika eneo la Sabasaba nje kidogo ya mji wa Musoma, mkoani Mara. 


Wamesema mabasi hayo ambayo yote yalikuwa kwenye mwendo kasi yalikutana kwenye daraja dogo katika eneo hilo huku pia gari dogo aina ya Land Crusser likitaka kuovateki na hivyo kupelekea kutokea kwa ajali hiyo. Mmoja wa mashuhuda hao aliyejitambulisha kwa jina la Juma Nyamhanga amesema alisikia kishindo kikubwa muda mfupi baada ya kutokea kwa ajali hiyo na baadae kusikia vilio vikitokea ndani ya mabasi hayo. 

Mwenyezi Mungu azilaze roho za maremu wote mahala pema peponi..
Akizungumzia kwa tabu akiwa amelazwa kwenye wodi namba 4 hospitali ya rufaa ya mkoa wa Mra, Frolence amesema walishangaa kuona abiria waliokuwa wamekaa mbele wakisimama na kurudi nyuma na ghafla akasikia mlio mkubwa. 

Akizungumza na Redio kahama fm nje ya chumba cha (ICU) kwa niaba ya Mganga Mkuu, Dakatari Martini Khani amethibitisha kutokea kwa ajali hiyo na kudai kuwa wamepokea idadi kubwa ya maiti na majeruhi huku idadi kamili ikiwa bado haijafahamika.

Jiunge na mi kwa kubonyeza kwenye link zifuatazo chini ili kupata habari mpya zaidi. 
          FACEBOOK >>> TWITTER  >>> MATUKIO KWA NJIA YA SAUTI
Usikose kuangalia Movies mbalimbali kutoka kila kona ya dunia, bofya kwenye picha iliyopo hapo chini kuona izo muvies
Nobody is a total failure if he dares to try to do something worthwhile. Tough times never last, but tough people do. The place broke up with applause. Those thirty - five hundred farmers who had lost hope and had battled depression found that hope.

Share habari hii kadri uwezavyo.

Contact us on mutalemwa.oesmo@gmail.com. Powered by Blogger.
© Copyright Mutalemwa Blog
Back To Top