Featured

    Featured Posts

    Social Icons


Loading...

FAHAMU KIUNDANI ZAIDI JUU YA UGONJWA WA EBOLA

Naomba nikushirikishe na wewe pia kwamba kuna mambo mengi na mazuri ndapi ya picha iliyopo hapo chini ibofye uone.
Ebola ni nini?
Ugonjwa wa Ebola pia  hujulikana  kama Ebola  Haemorgic Fever husababishwa  na virusi  vya  Ebola. Ebola  ni jina la mto  katika  nchi ya  Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, kijiji kimoja kati  ya vijiji viwili vya   kwanza   ugonjwa  huo   kugundulika  ilikuwa eneo  hilo mwaka 1976 . Kijiji  kingine kilikuwa  Sudan. Ebola ni ugonjwa wa hatari sana  ambao  huanza  ghafla  baada  ya  kugusana na wanayama    au mizoga katika  maeneo  ya misitu  ya mvua  ikiwa ni pamoja na  sokwe, nyani, popo, swala  na wengine . Ugonjwa  huu  unaua hadi 90% ya wale ambao wameathirika.
Je huambukizwaje? 
Virusi wa Ebola  huambukizwa toka kwa  mtu  mmoja  kwenda  kwa mwingine  kupitia  damu au majimaji  mengine  ya mwili , lakini pia vitanda, shuka, nguo au vitu vingine vilivyogusana na mgonjwa iwapo vimeguswa. Taratibu za  mazishi ambazo uhusisha kugusa mwili pia ni hatari. Virusi huingia mwilini kupitia kwenye vidonda au ngozi nyepesi.


Kundi lililo katika hatari zaidi ni wafanyakazi wa afya, na wale  wanaotunza watu  walioathirika na Ebola. Wanapaswa  kuvaa  nguo za kuwakinga mwili mzima  ikiwa ni pamoja na mask, miwani ya usalama, na wanapaswa kubadilika mipira  ya mikinoni  kati ya mgonjwa mmoja na wa pili.

Dalili  zake  ni zipi? 
Dalili za awali  ni  homa ya ghafla, udhaifu mkali, maumivu ya misuli, kuumwa na kichwa na koo. Dalili  hizo  hufuatiwa na Kutapika na kuharisha,hivi huongeza hatari ya mgonjwa kumwambukiza mtu mwingine. Figo na ini vinakuwa vimeathirika hivyo  magonjwa  anaweza  kutokwa na damu ndani na nje ya mwili,  hii ndio  maana  ukaitwa  Ebola  Haemorgic Fever. Wagonjwa huanza  kuambukiza mara tu  dalili zinapojitokeza, ambayo huwa  ni kati ya  siku mbili hadi 21 tangu kupata  maambukizi.


Matibabu  yake  ni yapi?
Kuna matibabu kidogo sana. Wagonjwa lazima  walazwe  katika  Chumba  cha uangalizi  maalum, na matibabu  huwa  ni kuongezewa maji  kwa njia  ya  mishipa au maji  ya  chumna  au kunywa maji ya chumvi chumvi. Wahudumu  pamoja  na  watu  wanaokuja  kuwa tazama lazima   wavae  mavazi  ya Kuwakinga  mwili  mzima  Ugonjwa  huu  hauna  tiba  wala  chanjo .  Hata hivyo   utafiti unaendelea    kutafuta chanjo.

Kwa nini ni hakuna tiba?
Imeonekana kuwa ni vigumu sana kupata madawa ya kutibu magonjwa ya virusi  kutoka kwa wanyama, kama  homa ya  mafua  ya ndege  na VVU. Ingawa kiwango cha vifo kiko juu, pia milipuko ya ebola imekuwa  ikatokea  mara  chache  na yote  imekuwa  ikidhibitiwa  kila wakati.  Hakuna soko hivyo uwezekano  wa kupata  faida  ni mdogo makampuni ya madawa  yanasita   kuwekeza katika utafiti na maendeleo ya dawa  za Ebola.


Kwanini  unatokea  tena  baada  ya  kudhibitiwa? 
Ugonjwa huu  unaweza  kudhibitiwa  kwa binadamu  lakini  si katika  hifadhi  yake  kwa  wanyama  na popo.  Hivyo  binadamu  anapogusana  na mnyama  aliyeathirika  hupata  maambukizi  tena.

Jiunge na mi kwa kubonyeza kwenye link zifuatazo chini ili kupata habari mpya zaidi. 
          FACEBOOK >>> TWITTER  >>> MATUKIO KWA NJIA YA SAUTI

Usikose kuangalia Movies mbalimbali kutoka kila kona ya dunia, bofya kwenye picha iliyopo hapo chini kuona izo muvies
Nobody is a total failure if he dares to try to do something worthwhile. Tough times never last, but tough people do. The place broke up with applause. Those thirty - five hundred farmers who had lost hope and had battled depression found that hope.

Share habari hii kadri uwezavyo.

Contact us on mutalemwa.oesmo@gmail.com. Powered by Blogger.
© Copyright Mutalemwa Blog
Back To Top