Featured

    Featured Posts

    Social Icons


Loading...

Kutoka CHETA KAZOLE kwenda VIKINDU GETINI ni 6.749Km Pekee.

Ukweli ni kwamba kutoka Vikindu Getini kwenda kijiji cha Kazole sio mbali, ni wastani wa 6.749Km au 7Km pekee kutoka Vikindu getini hadi Kazole kwenye kitongoji cha Cheta.

Ila panaonekana kuwa mbali kutokana na ubovu wa miundombinu iliyopo ikiwemo ubovu wa barabara, ukosefu wa umeme, hospital/ Zahanati nk.

 Leo naomba niupongeze uongozi wa kijiji cha Kazole kwa kuchonga Barabara yenye urefu wa wastani wa 4Km kutoka Kazole Magenge 20 hadi kitongoji cha Cheta. 

Zoezi ili lilianza juzi tarehe 21/2/18 na kumalizika jana tarehe 22/2/18.
 Kuchonga na kufunika Mashimo kwenye baadhi ya maeneo ya barabara hii kutasaidi kwa namna moja au nyingine kwa Magari yanayotoa huduma kwa abiria kutoka Vikindu mpaka Magodani. 
Maoni yangu nikwamba mmefanya vizuri kuchonga hii barabara lakini mnaonaje ikawekwa kifusi au Changarawe ili kuifanya iwe imara zaidi ili kuwaondolea adha ya usafiri wakazi wa Kazole, Cheta na Magodani kwa kipindi cha mvua kinacho karibia kuanza mwezi ujao? 

NI AIBU KUONA VINYESI MAENEO YA POSTA

Ndugu mdau karibu sana kwenye ukurasa mpya kabisa unaoitwa Kero Yangu. Ukurasa  huu utakuwa ukichapishwa kupitia Mutalemwa Blog pamoja na Tazama line.

Lengo la ukurasa  huu nikutazama pale palipo sahaulika na kuwakumbusha wahusika ili wakapafanyie kazi. Pia ukurasa huu hauishii hapa Dar es salaam tu, bali mpaka mikoani.

kwaiyo kama kuna jambo ambalo halijawekwa sawa na wahusika iwe ni Serikali,  watu binafsi au taasisi mbalimbali waweza kuwasilisha kero yako na sisi tutaichapisha mtandaoni ili iweze kupatiwa ufumbuzi wakudumu kutoka kwa mlengwa/walengwa/muhusika/wahusika.

Na kwakuanza leo tunajikita katikati ya jiji la Dar hapa maeneo ya Posta mpya. 

Leo nikiwa katika pitapita zangu kwenye mitaa ya posta mpya jijini Dar es salaam,  nimejisikia vibaya sana huku nikiwa nimegubikwa na aibu kubwa baada ya kukutana na station chemba

katikati ya barabara ya Kisutu ikiwa inatoa maji yenye vinyesi na kusambaza maji hayo mtaani, huku harufu mbaya ikitanda eneo lote linalozungukwa na maji hayo machafu.

Huku barabara ikiwa inatumiwa na watu mbalimbali wakiwemo viongozi mbalimbali wa nchi hii, wakati barabara izi zikiwa na mashimo makubwa.
Kiukweli inasikitisha sana maeneo ya posta kuwa katika hali kama hii, ambapo ndipo panatakiwa kuwa mfano wa kuigwa kwa sababu maghorofa makubwa na sehemu ambapo panapatikana bidhaa original ndio huku bila kusahau maofisi ya watu maarufu nk.

Nawaomba wahusika kwenye eneo zima la posta mpya jijini Dar es salaam muweze kurekebisha maeneo yote yenye kudhalilisha na kuaribu sifa ya eneo hili maarufu jamani.
Pia ikumbukwe kuwamba sio maeneo haya pekee bali yakomengine mengi zaidi ila kwa leo naishia hapa. Endelea kutembelea Mutalemwa Blog kwa habari zenye tija kwa jamii yetu.

Kwa maoni/ushauri au kero yako basi waweza kutuma ujumbe wako kwa sms au what's up  kupitia 0659919292 kumbuka kutaja majina yako kamili na sehemu ulipo kisha ujumbe wako tutauchapisha na utawafikia wahusika. 
Contact us on mutalemwa.oesmo@gmail.com. Powered by Blogger.
© Copyright Mutalemwa Blog
Back To Top