Mbali ya kupingwa kwa habari ya juzi iliyokuwa ikisema Raisi wa Burundi Pierre Nkurunziza amepinduliwa. Kiongozi wa Mapinduzi ya kijeshi Meja Jenerali Godefroid Niyombare alitoa taarifa hizo kupitia kituo cha radio kiitwacho Isanganiro radio akisema serikali ya Nkurunziza imevunjwa.
Alisema kuwa wananchi wa Burundi wamekuwa wakipinga vikali hatua yake ya kuwania muhula wa tatu. Jenerali huyo alifukuzwa kazi nchini buruundi kama mkuu wa ujasusi mwezi February.
Napenda kuchukua nafasi hii kuwapongeza sana wana Burundi wote kwa msimamo wao walioweza kuusimamia toka mwanzo mpaka sasa, pia nitoe wito kwa watu wote kwamba hakuna marefu yasiyokuwa na ncha, wananchi wakiamua kufanya jambo linawezekana kabisa.
Tukumbuke kuwa huwezi kuwaongoza watu kama hawakutaki, kwaiyo ushauri kwa Pierre Nkurunziza nikwamba akubali kuachia ngazi ili atawale Kiongozi ambeye wana Burundi wanamtaka kuliko kug'ang'ania nafasi iyo huku raia wakiendelea kupoteza maisha yao.