Mkazi wa kijiji cha Chibwechagula Mkoani Dodoma Ruth Matonya mwenye umri wa miaka 26 amejifungua mtoto wa ajabu ambaye nusu ya sura yake inafanana na chura na nusu nyingine inafanana na binadamu.
Mtoto huyo alizaliwa katika kituo cha afya cha Mtakatifu Luka kinachomilikiwa na kanisa la Anglikana alifariki dunia muda mfupi baada ya kuzaliwa.
Kwa mujibu wa Mganga mfawidhi wa hospitali hiyo Edwin Kihura alisema mara baada ya mama huyo kufika katika kituo hicho alikua na uchungu ambao haukua na kikomo lakini alishindwa kujifungua kwa njia ya kawaida licha ya njia ya uzazi kufunguka.
Alisema kutokana na hali hiyo iliwalazimu kumfanyia upasuaji mama huyo kwa lengo la kuokoa maisha yake na mtoto na mara baada ya upasuaji waliweza kutoa mtoto mwenye jinsia ya kike ambaye alikua na sura isiyoeleweka na sura yake nusu ilikua na binadamu na nyingine ya chura.
![](https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgqkfvdsCQnPtVtdB1BRo8WNnIXPkLftFAgnwnEsIn6wi5e6a3eWRGwII7wh1RRZiR7YnhR6IfHZu2S-L5TKd4i4JeqIXAZnEeqqNhmqdzjNYA4Q76BTKpB9MmvWIsr0dnAZXNg5DJSgT0/s200/FLASH+NECTA.gif)
Kwa habari za Matukio Kitaifa, Kimataifa, Michezo na Burudani, Ungana nami kupitia Link zifuatazo hapo chini.
In order you follow me just click one of the Icon Button above.