Featured

    Featured Posts

    Social Icons


Loading...

DARAJA LA MANDELA

Naomba nikushirikishe na wewe pia kwamba kuna mambo mengi na mazuri ndapi ya picha iliyopo hapo chini ibofye uone.
MAKALA
Daraja la Mandela; Kivutio kikuu Johannesburg

KWA UFUPI
Likiwa na urefu wa mita 248, daraja hilo linapamba anga la Johannesburg kwa rangi za upinde wa mvua hasa nyakati za usiku.
     
Jo’burg, Afrika Kusini. Tangu kuanza kuumwa kwa Nelson Mandela, watu mbalimbali wamekuwa wakifuatilia mambo mbalimbali yanayohusu maisha yake, mambo yote aliyoyafanya.

Wapo wengine wanaofuatilia kwa karibu hali yake kiafya, ingawa hofu imekuwa maisha nchini humo baada ya kifo chake.
Hata hivyo, miongoni mwa vivutio vikubwa ni Daraja la Nelson Mandela jijini Johannesburg.

Hili ni daraja kubwa ambalo lilikamilika kujengwa mwaka 2003, lakini kwa sasa limegeuka kivutio kwa maelfu ya wageni na wenyeji wanaolitembelea, kupiga picha za ukumbusho.

Likiwa na urefu wa mita 248, daraja hilo linapamba anga la Johannesburg kwa rangi za upinde wa mvua hasa nyakati za usiku.

Kwa ufupi, daraja hilo linatumika juu ya njia ya reli inayounganisha vitongoji vya  Newtown na Braamfontein, jirani na eneo maarufu la kibiashara lililogharimu Rand 38-milioni.

Wabunifu wake walitaka kuongeza kitu katika uzuri wa jiji hilo la kisasa, kupendezesha eneo la katikati ya jiji hili kwa kulipa sura ya kuvutia.

Lengo lake likiwa ni kuunganisha kitongoji kinachokua cha Newtown na eneo la kibiashara la Braamfontein, pia kuwezesha kuyafikia maeneo hayo kwa urahisi wakati wote.

Ujenzi wake mwanzoni ulionekana kuwa changamoto kubwa kwa timu ya wabunifu na wahandisi wake kupita eneo ambako njia 42 za reli zinapishana bila kuingilia usafiri au kusababisha misongamano ya magari.

Kwa jumla, daraja hilo la  Mandela ambalo ni ubunifu wa Kampuni ya Dissing & Weitling, ndilo kubwa la waya Kusini mwa Afrika.

Liliandaliwa maalumu kuwa jepesi, likichanganya vyuma na vifaa vingine vya kuliwezesha kuwa jepesi kwa kadri inavyowezekana, lakini lenye nguvu ya kutosha.

Kulingana na mtandao wa Engineering News,  kiasi cha mita za mraba 4,000 za zege, tani 1,000 za vyuma zilitumika kwenye ujenzi wake na tani 500  zaidi ya vyuma maalumu vya kushikilia msingi wake.
Usikose kuangalia Movies mbalimbali kutoka kila kona ya dunia, bofya kwenye picha iliyopo hapo chini kuona izo muvies
Nobody is a total failure if he dares to try to do something worthwhile. Tough times never last, but tough people do. The place broke up with applause. Those thirty - five hundred farmers who had lost hope and had battled depression found that hope.

Share habari hii kadri uwezavyo.

Contact us on mutalemwa.oesmo@gmail.com. Powered by Blogger.
© Copyright Mutalemwa Blog
Back To Top